Jumatatu, 16 Septemba 2013

KIJANA WA MAANA YU KOJE?



KIJANA WA MAANA:

Katika kuendelea juu ya kuwa kijana wa maana mbali na kuwa na pesa tu na vitu vingi vinaonekana vya thamani kwa mwanadamu.tunapenda tena tuangalie katika kipengele kinachofuata.
                                          

                                              II.Maisha uliyopitia (mateso & shida)

Maisha ni mchangunuo wa mambo mbalimbali ambayo mwanadamu anapitia tena katika hali tofautitofauti ambayo mwanadamu anapitia kila maisha mtu binafsi aliyopitia uacha alama ndani ya moyo wako na kuwa ni elimu kwa mtu husika au uzoefu alioupata katika maisha yake.

Katika sayari ya dunia tuliyonayo sasa wapo watu amabao wanaishi maisha tofautitofauti katika hali nzuri/njema na hali mbaya/duni.pia wako watu walianzia hali njema baadae wakaishia pabaya na wengine wapo walioanzia katika hali mbaya baadae wakaishia katika hali nzuri/njema na wengine wamekuwa na mchanganyiko na hatimae wakaishia katika hali iliyo njema au iliyo mbaya, inategemea na familia uliyotoka pamoja na hayo pia kuna kundi la watu ambao maisha yao ni maumivu mwanzo mwisho.

Na maisha uliyoyapitia ndio leo uko vile ulivyo katika muonekano ulionao sasa wa huzuni au wa furaha.
Hakuna maisha ambayo uliyo yapitia mbali na wokovu yakawa na kibali kwa Mungu kwa namna yoyote haijalishi jamii inakukubali au haikukubali katika muonekano wowote wa dunia hii hauna kibali kwa Mungu bali ni vile Mungu anavyotaka tu ndivyo utaupendeza moyo wa Mungu.

Unapoishi maisha mbali na wokovu unakuwa unajifunza vitu vingi na kushiriki mambo ambayo yanawezekana kuonekana katika ubora wake katika jamii yako jua jambo lolote unalojifunza au kushiriki lina jenga mambo ambayo yataendesha maisha yako katika namna unavyoelewa.

Na pindi usipokuwa makini unaweza kujikuta katika hali tete ambayo itakusumbua katika maisha yako inaweza kuwa kikwazo kati yako na Mungu kwa kiasi kikubwa na yanaweza kuwa kikwazo kikubwa katika kuleta maendeleo yako katika maisha ya rohoni na ya mwilini.


Kama binadamu wakawaida kuna yako mambo uliyokuwa unayafanya unapokuwa pekee yako chumbani au mahali popote pa siri(kufanya mapenzi, kujichua, mawazo ya ukatiri na dhana ya kutaka kujiua)


I wathesalonike 4:3-5

Kuna muonekano ambao Mungu alikusudia katika kutimiza hazma yake katika kukuleta hapa dunia kuna namna ya wewe kuwa usiwe tu kiolela. Kama baba aliye makini anavyoweza kumwandalia mwanawe hatma njema ya baadae.

Luka 12:2-3

Muonekana wako wa awali unaonekana sasa kwa kuwa vile utakavyo ishi itategemea sana vile unavyoelewa na kukubaliana na hali uliyokuwa nayo hapo awali.

II Samweli 12:12

I Wakoritho 6:13-20

Mwanzo 8:21

Mambo yoyote yanapokuwa yakiendelea katika nafsi ya mtu husika na wakati wingine mtu huyu uweza kutekeleza yale yanayoendelea ndani yake.

Na pindi unapojaribu kutenda jambo hili kuna mambo yanazaliwa kutokana na tendo hilo ambayo yanakuwa na muonekano mbalimbali:

Hesabu 31:17-18
                   
                    i)kuna hali ya kushutuka pindi mambo hayo yanapotamkwa.
  
 ii) hofu na kutojiamini utawala na kuwa na nafasi katika maisha ya muhusika.
           
 iii) hali ya wasiwasi na mashaka juu ya magonjwa ya zinaa mathalani. Ukimwi ,kisonono na mengine mengi.
          
 iv) wengine wana kuwa na hali ya ukimya na wengine inawatokea hali ya kupenda kuongea pasipo sababu.
         
 v) kuchukia haina ya jinsia inaweza kuwa ya kike au ya kiume.
          
vi) mawazo sugu ambayo yamekosa muafaka.
         
vii) kutoa mimba( lina hasara kubwa katika maisha ya mtu husika)

Ni vizuri kutafakari wapi umetoka na je! Unaenda wapi na je! Utafika je, hiyo safari yako uwezekano wa kufika upo kwa kiasi gani na uko tayari katika chngamoto mbalimbali katika kufikisha ile hatma yako.

Ni vizuri kutambua kuwa unahitaji neema ya Mungu katika kukufikisha pale ambapo yeye mwenyewe amepanga na kukusudia ya kuwa wewe upate kufika mahali husika na sio pale ambapo unatamani wewe tu.

Hii iko wazi ujana ili uweze kuwa mzuri au mbaya unategemea sana nani ni kiongozi wako katika kuongoza maisha yako.

Yohana 10:10
Mbali na Mungu hakuna ujana ulio salama kama ujampa yesu maisha yako kwa ukamilifu wake hauwezi ukawa salama.

Isaya 40:28-31
Hakuna mtu anajua jinsi unavyotakiwa kuwa isipokuwa Mungu anayejua wapi umetoka na wapi unaenda?

Yeremia 1:5
Mungu akisha kutambua inatosha sana haijalishi umetokea wapi bali vile Mungu alivyo kwako.

Zaburi 51:5


Prepared by ;
                     Nelson, Cothey – 0764 018 535 or cotheyn@yahoo.com
                    Katiti, James       - 0713 398 042 or james.adili19@gmail.com




“Itakuwa vizuru tukikutana tena katika wakati mwingine………..BARIKIWA

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni