Alhamisi, 3 Oktoba 2013

KIJANA WA MAANA YUKOJE?



KIJANA WA MAANA:

Katika kuendelea juu ya kuwa kijana wa maana mbali na kuwa na pesa tu na vitu vingi vinaonekana vya thamani kwa mwanadamu.tunapenda tena tuangalie katika kipengele kinachofuata.

iii.uhuru na uamuzi uliochukua

kila familia ina namna ya kuchukulia au kulea watu wake katika jamii hiyo kuna watu waliokuwa na uhuru na wengine waliokosa uhuru na wote kuna maamuzi waliochukua na hatimae wakawa jinsi walivyo.

Hakuna jambo ambalo linakaa katika moyo wako kwa muda mrefu kama maamuzi uliochukua halafu ukawekwa katika hali mbaya, kwakua katika mazingira haya hakuna wa kulaumiwa ila ni wewe binafsi.

Haijalishi ni shindikizo gani lilikusukuma hatimae ukaamua maamuzi uliyo yachukua bali kitakachoangaliwa hapo ni matokeo uliyo yachukua.

Yako maamuzi uliochukua pasipo kujua kwa usahihi wa jambo husika na kuna maamuzi uliochukua kwakua uliona ni sahihi kwa wakati ule lakini mwisho ukaujeruhi moyo wako.

Ezekieli 16:15-16,22-26

Unaweza ulipewa uhuru mkubwa nyumbani kwenu kwa lengo la wazazi kutaka uyafurahie maisha yako na uwafurahie wazazi wako lakini ukautumia ule uhuru katika maslahi yako pasipo kuangalia usahihi wa kitu naam kasha ukaona matokeo yake.

Kumbuka kwamba jambo ukisha lifanya linabaki kuwa historia katika maisha yako na wala haifutiki bali inabaki kuwa kumbukumbu ambayo inaweza kuwa na nguvu ndani ya maisha yako au isiwe na nguvu yote inakutegemea wewe binafsi.

Kunawezekana ulikuwa unakataa kutokana na mafundisho mazuri uliyofundishwa na wazazi wako nay ale uliyojifunza ukayafanya kuwa ni maisha yako lakini kutokana na maneno ya mtu akakushawishi hatimae 
ukaamua kukubaliana nae na hatimae ukaona matokeo yake yanaweza kuwa mabaya au mazuri inategemea na jambao lenyewe.

Mathayo 7:10-23

Yamkini hapo awali ulikuwa mtu mzuri sana hata wewe binafsi ulijitamani lakini ukakutana na rafiki mbaye kwa kiasi kikubwa alibadilisha maisha yako na kuwa kwa namna ya yeye ambayo ataifurahia (kutumia madawa ya kulevya(bangi,unga n.k), kujichua nawe ukakubaliana na njia hizo kumbe unajiharibu kisakolojia(akili).hata Mungu afurahi lakini kwa uhuru uliopewa ukaingia pengine hata bila ya kuruhusiwa hatimae matokeo ukayaona.

II petro 2:14-15

Waefeso 5:11-12


HAKUNA RAFIKI ATAKAYE  KUPENDA KATIKA HALI YOTE,
(pendo la weza kupungua hatimae kupotea kabisa. Yesu ndiye rafiki)


Yamuhimu:

I.rudi kwa Mungu(wokovu)

Mungu anakupenda vile ulivyo kwakua yeye ndie chimbuko la wanadamu lakini pindi utakapo okoka kwa Mungu unakuwa na kibali kwa Mungu cha tofauti.

Hata kama umepoteza mwelekeo jua kwamba ndani ya Mungu kuna mwelekeo sahihi ambayo ukimwamini basi utapata mwelekeo sahihi.

Mungu si kama wanadamu yeye afikiri kuhukumu bali ufikiria namna gani ya kukutoa mahali ulipo na kwenda mahala pengine penye ubora wako katika maisha yako.

II nyakati 33:1-3,11-13

Ona ni kweli ulikuwa unamtenda Mungu dhambi ya wazi au ya silini kiri kuwa wewe ndiye ambaye ulimkosea Mungu na sasa umeamua kurudi kwa moyo wote pasipo kuangalia kushoto wala kulia.

Mitahali 28:13

Onyesha ya kwamba unamwitaji Mungu kuliko chochote kwakua ni ndani yake tu ndiko kuliko na usalama na sio mahala pengine na ukijua lile alilopanga Mungu ndilo litakalo timia na sio alilopanga mpenzi wako wala wewe binafsi kwa hiyo Mungu kiwa upande wako kila kitu kitakuwa sawa.

Onyesha hali ya kumwitaji Mungu kwakua yeye anaweza kubadilisha leo ikawa kesho na kesho ikawa leo hivyo anauwezo wa kubadilisha historia yako akakupa historia nyingine iliyo bora zaidi ya vile unavyofikiria.
Tambua ulitumia mwili wako visivyo na wakati wako lakini sasa umeamua kutoa mwili wako kwa ajili ya Mungu peke yake.

I wakorintho 6:19

II wakorintho 7:9-10



Prepared by ;
                     Nelson, Cothey – 0764 018 535 or cotheyn@yahoo.com
                    Katiti, James       - 0713 398 042 or james.adili19@gmail.com




“Itakuwa vizuru tukikutana tena katika wakati mwingine………..BARIKIWA



Hakuna maoni:

Chapisha Maoni