Jumatano, 4 Desemba 2013

VIGEZO VYA KUPENDWA NA MUNGU



VIGEZO  VYA  KUMPENDA  MUNGU (UTHIBITISHO)

Hili ni jambo la kawaida sana kwa mtu yeyote mtu utakaye mpenda lazima awe na sifa ambazo wewe unazozitaka na wala haiwezi kutokea wewe hali ya kupenda penda hovyohovyo mtu asipite mbele zako.

Mungu apendwi kwa kuwa umejisikia kumpenda au umeona tu ipo haja ya kumpenda kwa wakati Fulani,bali viko vitu ambavyo Mungu akiviona anajua tu wewe sasa umeamua kumpenda kwa dhati sio unajaribu kumpenda.Katika kitu kizuri Mungu hashawishiki kwa maneno ya kawaida tu bali moyo unao jua unachofanya ndio unao mtisha Mungu.

Sio kwa vigezo vyako ndio ukaweze kumshawishi Mungu akupende bali ni kwa vigezo vyake, ikiwa kwa ni kwa vigezo vyako basi utajipenda mwenyewe na kama kwa vigezo vyake basi yeye atakupenda.

i.maisha ya kuacha vyote kwa ajili ya kristo kwa ukamilifu

unapoamua kumfuata yesu uyashikilie hayo maamuzi ulio yachukua na moyo wako ukushuhudie pasipo shaka ndani yako.

Ni jambo la muhimu kwa watu wanao amua kupendana ili waweze kuzidi na kushamili lazima asiwepo mtu mwingine akawa na nafasi sawa ndani yenu kama mlivyo.

Hali ya kuacha vyote haimaanishi kwamba uache kusoma kama unasoma,kuacha kazi kama unafanya kazi  au una fanya shughuli yeyote ya halali ukaiacha sivyo.

Bali ni vile moyo wako unavyo yapa kipaumbele/uzito mambo ambayo yanamfanya Mungu kuzidi ndani ya maisha yako.

Tamani sana maisha yako yawe na muunganiko wa kweli na Mungu yenye utiisho,mamlaka na nguvu pamoja na ushindi.

Tamani kuona maisha yako yakimuonyesha Mungu katika mwenendo mzima ulionao watu waone huruma,upendo,uponyaji,uweza wa Mungu penda kuona Mungu akiyafurahia maisha yako kuliko mtu yeyote hata mpenzi wako.

Mathayo 16:24-25

Kubali yote ya kukute lakini kamwe yasivuruge Mungu katika maisha yako yakaleta utengano wako na Mungu.

Yohana 16:27


ii.maisha ya kuangalia Mungu anakuonaje na wala sio wanakuonaje?

Siku zote motto mwenye akili uangalia wazazi wake wapendacho na si majirani wanachosema kwakua utambua furaha ya wazazi ndio furaha yake.

Mithali 10:1

siku zote watu wanakuona vile unavyoonekana hawa wezi kukuongeza au kukupunguza bali nafasi yao ni kusema katika hali ya kukosoa au kupongeza kulingana na mtazamo wake.

Una haja ya kuogopa hao bali unao nafasi ya kuwasikiliza na kuwa heshimu lakini mmbo mengine yote yana baki ndani yako binafsi kwani wewe ndio unajipenda hasa kuliko mwingine.

Maisha yasiyo ambatana na hofu ya kibinadamu bali ni hofu ya Mungu iliyo katika hali ya kupenda tena kwa furaha.

Maana Mungu katika wengi anakuangalia wewe binafsi hivyo katika wengi muangalie yeye binafsi.

Mhubiri 7:26(b)
Luka 12:22-24

iii.maisha yasiyo tazama aibu ya sasa bali aibu ya baadae(aibu ya milele)

Ishi maisha ya kutopata aibu ya milele kuliko aibu ya sasa isiyo dumu, hatima ya wanadamu iko mikononi mwa MUNGU.

Mathayo 10:32-33
Luka 12:20-21

Hakuna kisichikuwa na mwisho katika ulimwengu huu bali ni NENO  LITOKANALO KINYWANI  MWA  MUNGU.

Ishi isha ambayo kishindo cha mbingu kitaitikia na kukukubali na kusema kweli wewe ni mtu uliye amua kumpenda Mungu.

iv.maisha ya kufungwa nira ya kristo

haya ni maisha ya kumjua zaidi kristo kuliko chochote kwa kuwa ndicho kilichopewa nafasi kubwa ndani ya moyo mwake.

Unaposikia kitu kinachoitwa Mungu moyo wako unashtuka haoni nafasi ya kutulia kwa kuwa hauoni jambo ambalo litazuia kitu chochote kitazuia upendo wako kwake.

Moyo wako hutamani/haupendi kuona akisijisikia vibaya kwa ajili yako wewe unatamani kuona siku zote anakuwa na furaha pindi anapoona uwepo wako.(wewe ndio furaha yake)

Matendo 15:26
Mathayo 11:28-30

Utayari wako uwe kwaajili ya Mungu tu kwa ukamilifu wote mtumikie bwana wako pasipo shaka yoyote tena katika hali ya furaha isiyokoma.

Matendo 21:13

v.maisha ya kujenga mwili wa kristo

Na wala sio maisha yanayowaza kwa ajili yake binafsi bali ni mawazo yaliyojaa nimfanyie nini Mungu leo kizuri kuliko jana, hii ni hali muhimu sana kwa watu wanaopendana uwa wanawaza kwa ubora siku kwa siku unaongezeka.

Unatamani kuona furaha yake ikizidi siku hadi siku na sio ipungue ili linakuwa ni jukumu lako kwa kuwa UNAMPENDA.

Huu ndio moyo ambao Mungu anautafuta ambao utasimamisha ufalme wake na kuimalika na kuwa wakumu usio tikisika milele.

Mathayo 16:18
Waefeso 4:11-12

Unajenga mwili wa kristo kwa njia ya PENDO LA MUNGU NDANI YAKO.

Imeandaliwa na ;
                     Nelson, Cothey – 0764 018 535 or cotheyn@yahoo.com
                    Katiti, James       - 0713 398 042 or james.adili19@gmail.com

KILA LA KHERI…………..RAFIKI


Hakuna maoni:

Chapisha Maoni